• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kwimba District Council
Kwimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Orodha ya viongozi
      • Orodha ya wenyeviti wa Halmashauri
      • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Orodha ya wakurugenzi
    • Muundo wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na Usafi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Taka na Usafi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Utamaduni, Michezo na Sanaa
      • Kitengo cha Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • TEHAMA
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
      • Elimu
    • Elimu
    • Mkataba wa Hduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari
  • Machapisho
    • Fomu
  • Investment Opportunity
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika

DC ANG'AKA AWATAKA WATUMISHI WASIOTAYARI KUFANYA KAZI WAJIONDOE KWENYE UTUMISHI.

Posted on: December 16th, 2020

Mkuu wa Wilaya ya Kwimba Mhe.Senyi S.Ngaga amewataka watumishi wasioweza kufanya kazi kwa kasi ya awamu ya tano wajiondoe kwenye Utumishi ili wawekwe watu waliotayari kufanya kazi,DC ameyasema hayo kwenye kikao cha kamati ya ushauri ya Wilaya kilichofanyika jana tarehe 15/12/2020 kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Kwimba.

Katika kikao hicho wakuu wa Idara na viongozi wa Taasisi mbalimbali waliweza kuwasirisha Taarifa zao za miradi ya maendeleo.Akiwasirisha taarifa yake Meneja wa TARURA Eng Dickson L.Mwangwa amesema Serikali inayo mikakati ya kufungua barabara mpya,kukarabati barabara mbovu na kutengeneza madaraja ili kuondoa adha wanayoipata wananchi pindi mvua zinaponyesha baadhi ya madaraja yanafurika maji.Pamoja na hayo wajumbe wakataka kujua mkakati wa Serikali kuhusu Kujenga barabara ya rami ya kutoka Hungumalwa- Ngudu- Magu, hapo Katibu Tawala wa Wilaya Ndug. Ally Nyakia akajibu kuwa Serikali imeshafanya upembuzi yakinifu na wakati wowote barabara hiyo itajengwa.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba Bib.Pendo Malabeja


Meneja TARURA Eng. Dickson  Mwangwa



Mkuu wa Chuo Cha Maendeleo ya Wananchi Malya Ndug. Frank Josephat


Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Malya Ndug. Frank Josephat akatumia nafasi hiyo kuwaomba wajumbe wa kikao kukitangaza Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Malya kuwa ni chuo cha Serikali na kinatoa mafunzo ya ufundi umeme,ufundi bomba,ushonaji,ufundi wa magari(makenika) na Elimu ya Sekondari kwa wasichana waliokatizwa ndoto za kusoma kwa kupata mimba,kulazimishwa kuolewa na sababu nyingine wanasomeshwa bure,pia Mkuu wa Chuo amewaomba wananchi wote wenye vijana waliohitimu kidato cha nne na ambao hawakusoma Sekondari wote kwenda kusoma Chuoni hapo kwani kila mtu anapata mafunzo kulingana na kiwango chake cha Elimu.

Katika kikao hicho kiongozi wa Shirika la Reli Wilaya ya Kwimba amewashauri wananchi kutumia usafiri wa treni kwani treni ya mwendo kasi inakaribia kuanza kujengwa inayopita Wilayani hapa na kwa bahati mzuri kutakuwa na Kituo kikubwa (station) hapa Wilayani Kwimba eneo la Nkalalo (Bukwimba) na Kituo hicho kitakuwa cha abiria na mizigo hivyo amewataka abiria na wafanyabiashara wote kuwa tayari kutumia usafiri huo.

Aidha Mkuu wa Wilaya amewasisitiza wajumbe wa kikao hicho kuwa maendeleo ya Wilaya hii hayataletwa na watu wengine bali ni wananchi wote na viongozi kila mtu akitimiza wajibu wake Wilaya ya Kwimba itasonga mbele sana.

Matangazo

  • TANGAZO LA MNADA April 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WANAWAKE,VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 07, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA MAGARI NA PIKIPIKI February 20, 2025
  • TAHADHARI YA KIPINDUPINDU September 12, 2024
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • WANAFUNZI WAHIMIZWA KUSOMA KWA BIDII

    March 21, 2025
  • MKUU WA WILAYA AHIMIZA USAWA WA KIJINSIA NA UWAJIBIKAJI

    March 06, 2025
  • WATENDAJI WATAKIWA KUONGEZA JUHUDI ZA UKUSANYAJI MAPATO

    February 27, 2025
  • KWIMBA YATOA MILIONI 607 KWA VIKUNDI 37 VYA VIJANA,WANAWAKE NA WALEMAVU

    February 21, 2025
  • Onyesha zote

Video

ZIARA YA MHESHIMIWA DC TARAFA YA MWAMASHIMBA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2016
  • Orodha ya watumishi wenye vyeti vya kugushi
  • Orodha ya Madaktari waliojariwa April 2017
  • Ajira mpya za walimu wa Hisabati na Sayansi 2016/2017
  • Matokeo ya Kumaliza Kidato cha Sita na Ualimu 2017

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tovuti ya ofisi ya Rais utumishi wa umma
  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza
  • Tovuti ya ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Tume ya Maadili

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Mawasiliano

    Ngudu-Kwimba

    Sanduku la Posta: P.O.BOX 88

    Namba ya Simu: 0732 980528

    Simu ya Kiganjani: 0732980528

    Barua Pepe: ded@kwimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma zetu

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.