• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kwimba District Council
Kwimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Orodha ya viongozi
      • Orodha ya wenyeviti wa Halmashauri
      • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Orodha ya wakurugenzi
    • Muundo wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na Usafi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Taka na Usafi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Utamaduni, Michezo na Sanaa
      • Kitengo cha Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • TEHAMA
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
      • Elimu
    • Elimu
    • Mkataba wa Hduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari
  • Machapisho
    • Fomu
  • Investment Opportunity
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika

DC LUDIGIJA ATOA WITO WIZARA YA MIFUGO KUSIMAMIA NA KUFUATILIA DAWA ZA MIFUGO

Posted on: August 6th, 2024


Mkuu wa Wilaya ya Kwimba Mhe. Ng'wilabuzu Ludigija ametoa wito kwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuweka Kitengo maalumu cha ufuatiliaji na usimamizi wa dawa ya mifugo kama ilivyo kwa dawa za binadamu na vipodozi ili kuleta ufanisi katika uuzaji wa dawa za mifugo.


Mhe. Ludigija ametoa wito huo alipotembelea mabanda la Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba na mabanda ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi leo Agosti 06, 2024 katika viwanja vya Nyamhongolo yanapofanyika maonesho ya nanenane kwa Kanda ya Ziwa Magaharibi ambapo amewataka wataalamu hao kufikisha ujumbe huo katika ngazi ya juu wa ajili ya utekelezaji.


Mkuu huyo wa Wilaya amesema amekuwa akipokea malalamiko mengi ya wananchi kuhusu uuzwaji wa dawa za mifugo ambazo zimemaliza muda wake na hivyo kupelekea wananchi wengi kukosa imani na dawa hizo mwishowe kupoteza mifugo yao kutokana na magonjwa.


"Nimekutana na changamoto hii, wananchi wengi wanalalamika wanapewa dawa za kuosha ng'ombe ili kupe zife lakini hawaoni magonjwa hayo yakimalizika na Wataalamu wetu wamefatilia wamegundua dawa wanazouziwa wananchi hao ni feki na zingine zimekwisha muda wa matumizi".


Ni vizuri sasa wadau wetu wa mifugo kushirikiana na kuanza kufuatilia kwa karibu, kupita katika maduka hayo hata kwa kuanza na wale wasambazaji wakubwa ili tuweze kunusuru mifugo ya wafugaji inayokufa kila siku kutokana na kukosa dawa sahihi. Ameongeza Mkuu huyo wa Wilaya.


Aidha DC Ludigija amewapongeza wananchi wanaoendelea kutembelea maonesho hayo na kuwataka kutumia elimu ya kilimo wanayoipata kupitia maonesho hayo kujiletea mafanikio lakini pia amewataka wananchi hao kuwapatia pia elimu hiyo wale ambao hawakupata nafasi ya kutembelea maonesho hayo ili kuleta tija na mageuzi ya kilimo.


Mhe. Ludigija ametembelea maonesho hayo kujionea pia hali ya  maandalizi ya kilele cha nanenane ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda na kutoa maelekezo kadhaa kwa waandaaji wa maonesho hayo ili kuboresha sherehe za kilele hicho.

Matangazo

  • TANGAZO LA MNADA April 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WANAWAKE,VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 07, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA MAGARI NA PIKIPIKI February 20, 2025
  • TAHADHARI YA KIPINDUPINDU September 12, 2024
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • WANAFUNZI WAHIMIZWA KUSOMA KWA BIDII

    March 21, 2025
  • MKUU WA WILAYA AHIMIZA USAWA WA KIJINSIA NA UWAJIBIKAJI

    March 06, 2025
  • WATENDAJI WATAKIWA KUONGEZA JUHUDI ZA UKUSANYAJI MAPATO

    February 27, 2025
  • KWIMBA YATOA MILIONI 607 KWA VIKUNDI 37 VYA VIJANA,WANAWAKE NA WALEMAVU

    February 21, 2025
  • Onyesha zote

Video

ZIARA YA MHESHIMIWA DC TARAFA YA MWAMASHIMBA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2016
  • Orodha ya watumishi wenye vyeti vya kugushi
  • Orodha ya Madaktari waliojariwa April 2017
  • Ajira mpya za walimu wa Hisabati na Sayansi 2016/2017
  • Matokeo ya Kumaliza Kidato cha Sita na Ualimu 2017

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tovuti ya ofisi ya Rais utumishi wa umma
  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza
  • Tovuti ya ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Tume ya Maadili

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Mawasiliano

    Ngudu-Kwimba

    Sanduku la Posta: P.O.BOX 88

    Namba ya Simu: 0732 980528

    Simu ya Kiganjani: 0732980528

    Barua Pepe: ded@kwimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma zetu

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.