• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kwimba District Council
Kwimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Orodha ya viongozi
      • Orodha ya wenyeviti wa Halmashauri
      • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Orodha ya wakurugenzi
    • Muundo wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na Usafi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Taka na Usafi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Utamaduni, Michezo na Sanaa
      • Kitengo cha Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • TEHAMA
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
      • Elimu
    • Elimu
    • Mkataba wa Hduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari
  • Machapisho
    • Fomu
  • Investment Opportunity
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika

KAMATI YA SIASA YA WILAYA YAKAGUA MAENDELEO YA UTEKELEZAJI WA MIRADI

Posted on: September 19th, 2023



Kamati ya Siasa ya Wilaya ikiongonzwa na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya Mheshimiwa Sabana Salinja wamekagua maendeleo ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ikiwemo miradi ya Elimu,Afya, Utawala na kikundi cha walemavu.


Wakikagua mradi wa ujenzi wa Shule mpya ya Msingi Mwalulyeho wameishukuru Serikali kwa kuona umuhimu wa kuleta fedha za kujenga Shule hiyo ambayo imeanza kutoa huduma tarehe 18 Septemba 2023, kukamilika kwa Shule hiyo kumewasaidia wanafunzi waliokuwa wanatembea umbali mrefu zaidi ya kilomita nane kitu kilichokuwa kinapelekea wanafunzi wengi hasa madarasa ya awali kushindwa kuhudhuria masomo yao.


Wajumbe hao wamekagua ujenzi wa Hospitali ya Wilaya, hapo wamepongeza wataalamu na viongozi wote walioshiriki kusimamia utekelezaji wa mradi huo, pia wamesisitiza huduma za Afya ziboreshwe zaidi ili idadi ya Wananchi wanaopata huduma hapo iongezeke


" taarifa imeonyesha kuwa tangu muanze kutoa huduma katika Hospitali hii mapato yameongezeka sasa nishauri huduma ziboreshwe zaidi ili watu waje kupata huduma kwenye Hospitali hii na mapato yaongezeke zaidi" amesema Mwenyekiti wa CCM Mhe. Sabana


Mkuu wa Wilaya ya Kwimba Mheshimiwa Ng'wilabuzu Ludigija ameshiriki ziara hiyo naye amemtaka Mkandarasi anayetekeleza ujenzi wa jengo la utawala kuongeza kasi ya ujenzi huo ili jengo likamilike na kuanza kutumika.


Katika ziara hiyo miradi ya maji inayotekelezwa na wakala wa maji na usafi wa mazingira vijijini ( RUWASA) imekaguliwa, wakandarasi wanaotekeleza miradi hiyo wametakiwa kuongeza kasi ya utekelezaji ili miradi ya ujenzi wa tangi la maji Ligembe na Nkalalo yakamilike na yaanze kutoa huduma kwa wananchi.


Miradi mingine iliyokaguliwa ni ujenzi wa mabweni manne,madarasa nane na matundu ya vyoo katika Shule ya Sekondari Mwamashimba, ujenzi wa kituo cha Afya Hungumalwa, kikundi cha walemavu Malemve, ujenzi wa daraja mto magogo, ujenzi wa kituo cha Afya Budushi, ujenzi wa mabweni mawili, madarasa manne na matundu ya vyoo sita Shule ya Sekondari Sumve na ujenzi wa Shule mpya ya Msingi Kadashi B mradi unaotekelezwa kwa milioni 540 fedha za mradi wa Boost.

Matangazo

  • TANGAZO LA MNADA April 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WANAWAKE,VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 07, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA MAGARI NA PIKIPIKI February 20, 2025
  • TAHADHARI YA KIPINDUPINDU September 12, 2024
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • WANAFUNZI WAHIMIZWA KUSOMA KWA BIDII

    March 21, 2025
  • MKUU WA WILAYA AHIMIZA USAWA WA KIJINSIA NA UWAJIBIKAJI

    March 06, 2025
  • WATENDAJI WATAKIWA KUONGEZA JUHUDI ZA UKUSANYAJI MAPATO

    February 27, 2025
  • KWIMBA YATOA MILIONI 607 KWA VIKUNDI 37 VYA VIJANA,WANAWAKE NA WALEMAVU

    February 21, 2025
  • Onyesha zote

Video

ZIARA YA MHESHIMIWA DC TARAFA YA MWAMASHIMBA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2016
  • Orodha ya watumishi wenye vyeti vya kugushi
  • Orodha ya Madaktari waliojariwa April 2017
  • Ajira mpya za walimu wa Hisabati na Sayansi 2016/2017
  • Matokeo ya Kumaliza Kidato cha Sita na Ualimu 2017

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tovuti ya ofisi ya Rais utumishi wa umma
  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza
  • Tovuti ya ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Tume ya Maadili

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Mawasiliano

    Ngudu-Kwimba

    Sanduku la Posta: P.O.BOX 88

    Namba ya Simu: 0732 980528

    Simu ya Kiganjani: 0732980528

    Barua Pepe: ded@kwimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma zetu

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.