• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kwimba District Council
Kwimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Orodha ya viongozi
      • Orodha ya wenyeviti wa Halmashauri
      • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Orodha ya wakurugenzi
    • Muundo wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na Usafi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Taka na Usafi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Utamaduni, Michezo na Sanaa
      • Kitengo cha Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • TEHAMA
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
      • Elimu
    • Elimu
    • Mkataba wa Hduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari
  • Machapisho
    • Fomu
  • Investment Opportunity
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika

KATIBU TAWALA, WAHITIMU TUMIENI UJUZI KUJIAJILI

Posted on: November 30th, 2025


Katibu Tawala wa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba, Mohamed Ngasinda, amewataka vijana wahitimu wa vyuo vya ufundi kutumia ujuzi walioupata kujiajiri na kuchangamkia fursa zilizopo ili kupunguza changamoto ya ukosefu wa ajira.


Akizungumza katika mahafali ya kwanza ya Chuo cha  ufundi stadi(VETA)wilayani humo,Ngasinda alisema Serikali imeendelea kuweka mazingira wezeshi kwa vijana na wanawake kupitia programu za mafunzo ya ufundi na ujasiriamali zinazochangia kuwajengea uwezo, kuwapatia mtaji na kuongeza kipato cha mtu mmoja mmoja pamoja na pato la taifa.


Ngasinda alisema jumla ya wahitimu 17 wamepatiwa mafunzo hayo ambayo yamefadhiliwa kupitia programu mbalimbali ikiwemo ya wanawake na Samia Scholarship, ambayo imelenga kuwainua wanawake kiuchumi kupitia kozi fupi za ufundi stadi.


“Wahitimu tayari mnazo fursa za kuzitumia katika soko la ajira. Nyinyi ni mafundi waliohitimu na mnaweza kuanzisha kampuni, miradi au vikundi vya ujasiriamali ili kujipatia kipato,” alisema.


Aliongeza kuwa Serikali inaendelea kutatua changamoto ya ajira kwa vijana kwa kuweka mifumo ya kuwawezesha, ikiwemo mikopo ya asilimia 10 inayotolewa kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.


Katibu Tawala huyo aliwataka wahitimu kutumia elimu waliyoipata katika kujiajiri kupitia fursa za ufundi kama umeme, mabomba na ujenzi, pamoja na kufungua maduka ya vifaa vya ujenzi na miradi mingine ya uzalishaji.


Alisisitiza kuwa hakuna lengo la vijana kukaa kusubiri mikopo pekee, bali kutumia wataalam wa maendeleo ya jamii kupata ushauri sahihi wa kuanzisha miradi.


Ngasinda pia amewataka vijana kuendelea kulinda amani na kuepuka kudanganyika na makundi yenye misukumo mibaya.


Mahafali hayo yamehudhuriwa na wahitimu 49 kutoka chuo cha Vefa, ambao wametakiwa kuwa mfano wa kuigwa katika jamii kwa kutumia ujuzi waliopata.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA 2025 KWIMBA November 05, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WANAWAKE,VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 07, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA MAGARI NA PIKIPIKI February 20, 2025
  • TANGAZO LA KITWA KWENYE USAILI October 14, 2025
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • WASIMAMIZI WA MIRADI WATAKIWA KUONGEZA KASI YA UTEKELEZAJI

    January 07, 2026
  • WANANCHI WAHAMASISHWA KUJIUNGA NA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    January 05, 2026
  • WANANCHI WAHAMASISHWA KUJIUNGA NA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    January 05, 2026
  • KWIMBA YAPANDISHA UFAULU ELIMU HADI ASILIMIA 93

    December 23, 2025
  • Onyesha zote

Video

ZIARA YA MHESHIMIWA DC TARAFA YA MWAMASHIMBA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2016
  • Orodha ya watumishi wenye vyeti vya kugushi
  • Orodha ya Madaktari waliojariwa April 2017
  • Ajira mpya za walimu wa Hisabati na Sayansi 2016/2017
  • Matokeo ya Kumaliza Kidato cha Sita na Ualimu 2017

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tovuti ya ofisi ya Rais utumishi wa umma
  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza
  • Tovuti ya ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Tume ya Maadili

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Mawasiliano

    Ngudu-Kwimba

    Sanduku la Posta: P.O.BOX 88

    Namba ya Simu: 0732 980528

    Simu ya Kiganjani: 0732980528

    Barua Pepe: ded@kwimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma zetu

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.