• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kwimba District Council
Kwimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Orodha ya viongozi
      • Orodha ya wenyeviti wa Halmashauri
      • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Orodha ya wakurugenzi
    • Muundo wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na Usafi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Taka na Usafi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Utamaduni, Michezo na Sanaa
      • Kitengo cha Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • TEHAMA
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
      • Elimu
    • Elimu
    • Mkataba wa Hduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari
  • Machapisho
    • Fomu
  • Investment Opportunity
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika

KIJIJI CHA HUNGUMALWA CHAPONGEZWA KWA UJENZI WA SEKONDARI

Posted on: August 9th, 2021

Wajumbe wa Kamati ya fedha,Uongozi na Mipango wawapongeza viongozi wa Kijiji cha Hungumalwa kwa maamuzi ya kujenga Shule ya Sekondari ya Kijiji chao, Wananchi wamezoea kujenga Shule za kata lakini katika Kijiji hiki imekuwa tofauti kwani wananchi wameamua kujenga Shule ya Kijiji chao baada ya kuona wanafunzi wao wanatembea umbali mrefu kwenda Sekondari ya Kata iliko.Pongezi hizo zimetolewa leo tarehe 09 Agosti,2021 huko Hungumalwa wakati Kamati hiyo ikifanya ziara ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo.

Aidha Shule hiyo imefunguliwa mwaka huu ambapo wanafunzi wa kidato cha kwanza wanaendelea na masomo katika madarasa matano yaliyokamilika huku wananchi wakiendelea na ujenzi wa madarasa mengine matano ambayo kwa sasa yamefikia hatua ya boma. Mwenyekiti wa Halmashauri Mheshimiwa Theleza Lusangija amewapongeza kwa hatua hiyo na amewashauri kuendeleza ushirikiano huo wenye tija kwa wananchi.



Katika ziara hiyo miradi ya Elimu na Afya imetembelewa ambapo katika Shule ya Sekondari Walla Maabara tatu zimekaguliwa na ukarabati wa Maabara hizo uko katika hatua za ukamilishaji huku milioni 42.7 zikiwa zimetumika kutoka Serikali kuu na nguvu za Wananchi.



Aidha Kamati hiyo imekagua ujenzi wa madarasa mawili na Ofisi katika Shule ya Msingi Igunguhya ambapo Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo ameshauliwa kusimamia kwa umakini shughuli zinazofanyika katika eneo lake la kazi ikiwemo ujenzi.

Kamati hiyo imekagua ujenzi wa Zahanati ya Sangu ambayo iko katika hatua za ukamilishaji huku milioni 79.8 zikiwa zimetumika kutoka Serikali kuu, Halmashauri na nguvu za Wananchi.Hapa kamati imeshauri ujenzi huo ukamilike haraka ili huduma zianze kutolewa mahali hapo.


Vilevile Kamati hiyo haikuishia hapo imeweza kukagua ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kwimba inayojengwa eneo la Icheja kata ya Ngudu.Hapa kamati imepongeza wasimamizi wa ujenzi huo kwa hatua iliyofikiwa ambapo majengo zaidi ya kumi yakiwa yamekamilika na mengine machache yako kwenye hatua ya ukamilishaji.



Matangazo

  • TANGAZO LA MNADA April 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WANAWAKE,VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 07, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA MAGARI NA PIKIPIKI February 20, 2025
  • TAHADHARI YA KIPINDUPINDU September 12, 2024
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • WANAFUNZI WAHIMIZWA KUSOMA KWA BIDII

    March 21, 2025
  • MKUU WA WILAYA AHIMIZA USAWA WA KIJINSIA NA UWAJIBIKAJI

    March 06, 2025
  • WATENDAJI WATAKIWA KUONGEZA JUHUDI ZA UKUSANYAJI MAPATO

    February 27, 2025
  • KWIMBA YATOA MILIONI 607 KWA VIKUNDI 37 VYA VIJANA,WANAWAKE NA WALEMAVU

    February 21, 2025
  • Onyesha zote

Video

ZIARA YA MHESHIMIWA DC TARAFA YA MWAMASHIMBA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2016
  • Orodha ya watumishi wenye vyeti vya kugushi
  • Orodha ya Madaktari waliojariwa April 2017
  • Ajira mpya za walimu wa Hisabati na Sayansi 2016/2017
  • Matokeo ya Kumaliza Kidato cha Sita na Ualimu 2017

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tovuti ya ofisi ya Rais utumishi wa umma
  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza
  • Tovuti ya ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Tume ya Maadili

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Mawasiliano

    Ngudu-Kwimba

    Sanduku la Posta: P.O.BOX 88

    Namba ya Simu: 0732 980528

    Simu ya Kiganjani: 0732980528

    Barua Pepe: ded@kwimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma zetu

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.