• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kwimba District Council
Kwimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Orodha ya viongozi
      • Orodha ya wenyeviti wa Halmashauri
      • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Orodha ya wakurugenzi
    • Muundo wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na Usafi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Taka na Usafi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Utamaduni, Michezo na Sanaa
      • Kitengo cha Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • TEHAMA
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
      • Elimu
    • Elimu
    • Mkataba wa Hduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari
  • Machapisho
    • Fomu
  • Investment Opportunity
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika

MIAKA 63 YA UHURU KWIMBA IMEPIGA HATUA KUBWA

Posted on: December 9th, 2024

 "tunapokuwa tunaadhimisha miaka 63 ya Uhuru tunajivunia amani na maendeleo ambayo Baba wa Taifa alianzisha na viongozi waliofuata  wanaendeleza, pia tunamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan  kwa kuendelea kutoa fedha za maendelo barabara,elimu ,afya na miradi mingine"

Kauli hii imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kwimba Mhe. Ng'wilabuzu Ludigija  wakati wa mdahalo uliokuwa ukijadili maendeleo katika sekta mbalimbali hapa Wilayani Kwimba baada ya Uhuru wa Tanganyika

" Serikali  imefanya kazi kubwa sana na hapa Kwimba tumepiga hatua kubwa kwa mfano barabara kutoka hapa ngudu kwenda Mwanza mjini tulisafiri zaidi ya masaa sita lakini kwa sasa barabara  zimeboreshwa sana tunatumia saa moja na nusu" Ludigija

Mkuu wa Wilaya amesisitiza kuwa Wilaya ya Kwimba kabla ya Uhuru kulikuwa na Shule tano tu lakini kwa sasa kuna shule zaidi ya 200 za msingi na Sekondari  hivyo maendeleo ni makubwa.

Akielezea kauli mbiu ya miaka 63 ya Uhuru inayosema "JITOKEZE KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025 KWA AMANI NA UTULIVU"  Pia ametumia wasaa huo kuwaasa wananchi kuwa tayari kushiriki uchaguzi Mkuu utakaofanyika mwaka 2025, ambapo amesisitiza amani na usalama katika kipindi chote.

Nao wazee maarufu waliokuwepo enzo za Uhuru ambao wameshiriki mdahalo  wameelezea jinsi Kwimba ilivyo na  maendeleo makubwa kwani miaka 63 iliyopita  hakukuwa na barabara za lami, hakukuwa na maji kila mahali, vituo vya afya vilikuwa vichache hata umeme haukuwepo walitumia vibatari, lakini kwa sasa vitu vyote vipo japo bado kuna changamoto chache.

Katika mdahalo huo wanafunzi kutoka Shule za sekondali wametoa hoja mbalimbali zikionyesha jinsi Taifa lilivyopiga hatua kwenye  miundombinu ya barabara, Elimu, maji Afya na Umeme na miradi mingine.

Aidha watu wenye mahitaji maalumu wameshiriki mdahalo huo ambapo nao wameishukuru Serikali kwa kuendelea kuwajali hasa kwa kuwapatia mikopo kwaajili ya vikundi vya ujasiliamari.

Matangazo

  • TANGAZO LA MNADA April 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WANAWAKE,VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 07, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA MAGARI NA PIKIPIKI February 20, 2025
  • TAHADHARI YA KIPINDUPINDU September 12, 2024
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • WANAFUNZI WAHIMIZWA KUSOMA KWA BIDII

    March 21, 2025
  • MKUU WA WILAYA AHIMIZA USAWA WA KIJINSIA NA UWAJIBIKAJI

    March 06, 2025
  • WATENDAJI WATAKIWA KUONGEZA JUHUDI ZA UKUSANYAJI MAPATO

    February 27, 2025
  • KWIMBA YATOA MILIONI 607 KWA VIKUNDI 37 VYA VIJANA,WANAWAKE NA WALEMAVU

    February 21, 2025
  • Onyesha zote

Video

ZIARA YA MHESHIMIWA DC TARAFA YA MWAMASHIMBA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2016
  • Orodha ya watumishi wenye vyeti vya kugushi
  • Orodha ya Madaktari waliojariwa April 2017
  • Ajira mpya za walimu wa Hisabati na Sayansi 2016/2017
  • Matokeo ya Kumaliza Kidato cha Sita na Ualimu 2017

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tovuti ya ofisi ya Rais utumishi wa umma
  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza
  • Tovuti ya ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Tume ya Maadili

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Mawasiliano

    Ngudu-Kwimba

    Sanduku la Posta: P.O.BOX 88

    Namba ya Simu: 0732 980528

    Simu ya Kiganjani: 0732980528

    Barua Pepe: ded@kwimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma zetu

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.