• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kwimba District Council
Kwimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Orodha ya viongozi
      • Orodha ya wenyeviti wa Halmashauri
      • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Orodha ya wakurugenzi
    • Muundo wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na Usafi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Taka na Usafi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Utamaduni, Michezo na Sanaa
      • Kitengo cha Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • TEHAMA
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
      • Elimu
    • Elimu
    • Mkataba wa Hduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari
  • Machapisho
    • Fomu
  • Investment Opportunity
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika

MKUU WA MKOA WA MWANZA AZINDUA MIUNDOMBINU YA MABWENI MWAMASHIMBA NA SHULE MPYA YA MWALULYEHO

Posted on: November 28th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla leo novemba 28, 2023 amezindua Miundombinu ya Kidato cha tano kwenye Shule ya Sekondari Mwamashimba wilayani Kwimba iliyogharimu zaidi ya shilingi Milioni 600.


Akizungumza na wanafunzi wa shule hiyo, Mhe. Makalla ameupongeza uongozi wa shule hiyo na halmashauri kwa usimizi mzuri wa Mabweni 3, Vyumba vya Madarasa 8 na Matundu ya vyoo 13 utakaosaidia kupunguza msongamano wa wanafunzi kwenye madarasa na mabweni.


"Nimeona mabweni mazuri yenye mpangilio mzuri wa vitanda, madarasa na matundu ya vyoo vyote kwenye hali ya usafi na unadhifu mzuri, tumieni jitihada hizi za uboreshaji kutulia na kusoma kwa bidii na nina imani baadae tutawapata viongozi wazuri kutoka kwenye shule hii." Makalla.


Vilevile, Mhe. Makalla ameagiza kulindwa kwa eneo la shule hiyo kwa kutambua na kuweka mipaka na kuweka uzio ili kuwalinda wanafunzi na kuepusha migogoro ya ardhi inayosababishwa na wananchi kuingia kwenye maeneo ya taasisi hususani yasiyo na mipaka inayofahamika.


Mhe. Ng'wilabuzu Ludigija amemhakikishia kiongozi huyo wa Mkoa kuwa ufaulu utaongezeka kwani pamoja na kuondoa msongamano wanafunzi kwenye shule hiyo watapata fursa nzuri ya kusoma kwenye mazingira mazuri ya kufundishia na kujifunzia.


"Mhe. Mkuu wa Mkoa wanafunzi wa kidato cha tano na sita wapo zaidi ya Mia 600 lakini kwa uwepo wa mabweni haya hivi sasa kila mwanafunzi atalala kwenye kitanda chake, hakuna tena msongamano bweni wala darasani." Amefafanua Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bi. Happness Msanga.


Katika hatua nyingine, Mkuu wa Mkoa amezindua Shule mpya ya Msingi Mwalulyeho katika kijiji cha Chasalawi Kata ya Bupamwa iliyojengwa kwa zaidi ya Milioni 250 ambayo imesaidia kuondoa adha ya kutembea umbali mrefu  kuelekea shule ya Chasalawi.


"Kama mlikua na kiu ya kupata shule, sasa mmejengewa tumeiona ni nzuri yenye samani za kutosha, basi waleteni watoto kwenye hii shule wasome maana hawa 303 wamehamia hivyo wazazi hakikisheni watoto wote wanakuja shule ifikapo mwezi januari 2024 asibaki nyumbani hata mmoja mweye umri wa kuanza shule" amesema Makalla


Matangazo

  • TANGAZO LA MNADA April 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WANAWAKE,VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 07, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA MAGARI NA PIKIPIKI February 20, 2025
  • TAHADHARI YA KIPINDUPINDU September 12, 2024
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • WANAFUNZI WAHIMIZWA KUSOMA KWA BIDII

    March 21, 2025
  • MKUU WA WILAYA AHIMIZA USAWA WA KIJINSIA NA UWAJIBIKAJI

    March 06, 2025
  • WATENDAJI WATAKIWA KUONGEZA JUHUDI ZA UKUSANYAJI MAPATO

    February 27, 2025
  • KWIMBA YATOA MILIONI 607 KWA VIKUNDI 37 VYA VIJANA,WANAWAKE NA WALEMAVU

    February 21, 2025
  • Onyesha zote

Video

ZIARA YA MHESHIMIWA DC TARAFA YA MWAMASHIMBA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2016
  • Orodha ya watumishi wenye vyeti vya kugushi
  • Orodha ya Madaktari waliojariwa April 2017
  • Ajira mpya za walimu wa Hisabati na Sayansi 2016/2017
  • Matokeo ya Kumaliza Kidato cha Sita na Ualimu 2017

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tovuti ya ofisi ya Rais utumishi wa umma
  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza
  • Tovuti ya ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Tume ya Maadili

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Mawasiliano

    Ngudu-Kwimba

    Sanduku la Posta: P.O.BOX 88

    Namba ya Simu: 0732 980528

    Simu ya Kiganjani: 0732980528

    Barua Pepe: ded@kwimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma zetu

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.