• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kwimba District Council
Kwimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Orodha ya viongozi
      • Orodha ya wenyeviti wa Halmashauri
      • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Orodha ya wakurugenzi
    • Muundo wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na Usafi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Taka na Usafi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Utamaduni, Michezo na Sanaa
      • Kitengo cha Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • TEHAMA
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
      • Elimu
    • Elimu
    • Mkataba wa Hduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari
  • Machapisho
    • Fomu
  • Investment Opportunity
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika

RC MTANDA WATAKA WAKULIMA KUZINGATIA KANUNI ZA UZALISHAJI WA ZAO LA PAMBA

Posted on: November 18th, 2024


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka wakulima wa pamba mkoani humo kung'oa na kuchoma moto mazalia ya Pamba ya msimu uliopita kabla ya Septemba 15 ya kila mwaka ili kutoathiri msimu mpya wa kilimo hicho.


Mhe. Mtanda ametoa agizo hilo mapema leo Jumatat  Novemba 18, 2024 wakati akifunga kikao cha viongozi ngazi ya wilaya kwa ajili ya kampeni ya ung'oaji wa masalia ya Pamba wilayani Kwimba.


Amesema kutofanya hivyo kunasababisha wadudu kuzaliana na kusubiri pamba mpya shambani kuiharibu, hivyo ili kujihakikishia uzalishaji wenye tija ni lazima wakulima wafuate kanuni za kilimo cha zao hilo kwa kusafisha mashamba mapema kabla ya msimu mwingine.


"Viongozi wote mpo hapa maafisa ugani, tarafa, kata na vijiji nawaagiza  muda wa hiyari umekwisha twendeni tukatekelze kanuni bora za kilimo cha Pamba kwani zao hili ndio injini ya uchumi wa wananchi wa Mwanza kwa miaka mingi." Mtanda.


Aidha, ameipongeza bodi na kwa kipekee balozi wa Pamba nchini,Aggrey Mwanri kwa juhudi zake za uelimishaji wakulima wa Pamba nchini na kwa kipekee mkoani Mwanza ambako kimsingi amechagiza uzalishaji na kufanya idadi ya wakulima waliopo mkoani humo kuwa sawa na waliopo kwenye mikoa 17 nchini.


Balozi wa Pamba Mhe. Agrey Mwanri amesema tatizo kubwa linalokwamisha Mbegu mpya kumea kwenye mashamba ya Pamba ni wakulima kutong'oa maotea ya pamba ya msimu uliopita kwani msimu mpya unachelewa na hatimaye mvua za vuli zinawapita.


Amefafanua kuwa mwisho wa kusafisha pamba ni tarehe 15 Septemba, 2024 ya kila mwaka ili msimu mpya uanze lakini wapo baadhi ya wakulima wamekua wakiacha maotea kwa lengo la kulisha mifugo kinyume na kanuni za kilimo bora na kupelekea kukwamisha uzalishaji.


"Mkiruhusu mimea ya msimu uliopita kuendelea kubaki shambani mtakua mnakaribisha wadudu kama Chawajani, Kandambili na ndio maana hivi sasa neema na baraka ya zao la pamba kwenye uchumi wa wananchi zimepungua kutokana na kushuka kwa takwimu za uzalishaji." Mwanri.


Aidha, amekemea tabia ya wakulima kuchanganya mazao na akatoa mfano wa Pamba na Mahindi yakioteshwa kwenye shamba moja yanasababisha zao moja kushiba rutuba.

Matangazo

  • TANGAZO LA MNADA April 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WANAWAKE,VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 07, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA MAGARI NA PIKIPIKI February 20, 2025
  • TAHADHARI YA KIPINDUPINDU September 12, 2024
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • WANAFUNZI WAHIMIZWA KUSOMA KWA BIDII

    March 21, 2025
  • MKUU WA WILAYA AHIMIZA USAWA WA KIJINSIA NA UWAJIBIKAJI

    March 06, 2025
  • WATENDAJI WATAKIWA KUONGEZA JUHUDI ZA UKUSANYAJI MAPATO

    February 27, 2025
  • KWIMBA YATOA MILIONI 607 KWA VIKUNDI 37 VYA VIJANA,WANAWAKE NA WALEMAVU

    February 21, 2025
  • Onyesha zote

Video

ZIARA YA MHESHIMIWA DC TARAFA YA MWAMASHIMBA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2016
  • Orodha ya watumishi wenye vyeti vya kugushi
  • Orodha ya Madaktari waliojariwa April 2017
  • Ajira mpya za walimu wa Hisabati na Sayansi 2016/2017
  • Matokeo ya Kumaliza Kidato cha Sita na Ualimu 2017

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tovuti ya ofisi ya Rais utumishi wa umma
  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza
  • Tovuti ya ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Tume ya Maadili

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Mawasiliano

    Ngudu-Kwimba

    Sanduku la Posta: P.O.BOX 88

    Namba ya Simu: 0732 980528

    Simu ya Kiganjani: 0732980528

    Barua Pepe: ded@kwimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma zetu

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.