• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kwimba District Council
Kwimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Orodha ya viongozi
      • Orodha ya wenyeviti wa Halmashauri
      • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Orodha ya wakurugenzi
    • Muundo wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na Usafi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Taka na Usafi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Utamaduni, Michezo na Sanaa
      • Kitengo cha Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • TEHAMA
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
      • Elimu
    • Elimu
    • Mkataba wa Hduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari
  • Machapisho
    • Fomu
  • Investment Opportunity
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika

SERIKALI YASEMA UPELELEZI UNAENDELEA KUJUA CHANZO CHA MOTO SUMVE

Posted on: November 22nd, 2025


'Tunatoa pole kwa wanafunzi wote waliopata changamoto ya kuungua mabweni yao kidato cha kwanza na kidato cha tatu, Serikali kupitia vyombo vyake vya usalama inaendelea kuchunguza chanzo cha moto"

Haya yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Bi. Johari Samizi ambaye amemuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mwanza katika tukio hilo, ambapo wanafunzi wameendelea kuhamasishwa na kutiwa moyo kutokana na janga la moto lilitokea katika Shule ya Sekondari Sumve ambapo mabweni mawili yaliteketea kwa moto tarehe 20,Novemba 2025

Mheshimiwa Johari ametumia wasaa huo kuwapongeza wananchi wa Sumve kwa moyo wa utu waliouonyesha siku hiyo ya tukio ambapo wananchi walihakikisha hakuna mwanafunzi anayezurika na moto

" tunawashukuru sana Wananchi wa Sumve mlionyesha moyo wa utu,watu walihatarisha maisha yao wakaingia kwenye moto kuokoa vitu vya wanafunzi, asanteni sana na niwaombe muendelee na moyo huo wa upendo na kujali" amesema Johari

Naye katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndugu Elikana Balandya ametumia nafasi hiyo kuwapa pole wanafunzi wote waliopata changamoto na amewashauri wasikate tamaa badara yake wawe wastahimilivu na walipokee hilo kama changamoto ambayo haiwezi kuwaharibia taratibu zao za masomo.

Aidha Balandya amewahakikishia wanafunzi hao ulinzi wa uhakika, hivyo wanapaswa kuendelea na masomo yao huku changamoto za vifaa na vitu vyote vilivyoungua vikiendelea kupatiwa ufumbuzi.

Aidha Mkuu wa shule hiyo Mwalimu Komenkesha ameushukuru uongozi wote kuanzia ngazi ya Mkoa hadi kijiji kwa kuendelea kusaidia kuimarisha ulinzi na kusaidia upatikanaji wa vifaa muhimu vya wanafunzi kama shuka,miswaki, kalamu na vifaa vingine.

Viongozi waliofika shuleni hapo wameahidi kutoa magodoro ya wanafunzi wote waliopata changamoto ya kuungua mabweni yao ili kuhakikisha wanafunzi hao wanalala vizuri na kupata muda wa kupumzika ili janga hilo lisiathiri muda wao wa kujisomea.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA 2025 KWIMBA November 05, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WANAWAKE,VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 07, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA MAGARI NA PIKIPIKI February 20, 2025
  • TANGAZO LA KITWA KWENYE USAILI October 14, 2025
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • KAIMU MKURUGENZI AFUNGUA MAFUNZO YA MPANGO NA BAJETI

    November 27, 2025
  • DAS AKABIDHI PIKIPIKI KWA MAAFISA UGANI

    November 25, 2025
  • WATUMISHI AJIRA MPYA WAASWA KUZINGATIA KANUNI ZA UTUMISHI WA UMMA

    November 24, 2025
  • SERIKALI YASEMA UPELELEZI UNAENDELEA KUJUA CHANZO CHA MOTO SUMVE

    November 22, 2025
  • Onyesha zote

Video

ZIARA YA MHESHIMIWA DC TARAFA YA MWAMASHIMBA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2016
  • Orodha ya watumishi wenye vyeti vya kugushi
  • Orodha ya Madaktari waliojariwa April 2017
  • Ajira mpya za walimu wa Hisabati na Sayansi 2016/2017
  • Matokeo ya Kumaliza Kidato cha Sita na Ualimu 2017

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tovuti ya ofisi ya Rais utumishi wa umma
  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza
  • Tovuti ya ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Tume ya Maadili

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Mawasiliano

    Ngudu-Kwimba

    Sanduku la Posta: P.O.BOX 88

    Namba ya Simu: 0732 980528

    Simu ya Kiganjani: 0732980528

    Barua Pepe: ded@kwimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma zetu

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.