• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kwimba District Council
Kwimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Orodha ya viongozi
      • Orodha ya wenyeviti wa Halmashauri
      • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Orodha ya wakurugenzi
    • Muundo wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na Usafi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Taka na Usafi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Utamaduni, Michezo na Sanaa
      • Kitengo cha Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • TEHAMA
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
      • Elimu
    • Elimu
    • Mkataba wa Hduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari
  • Machapisho
    • Fomu
  • Investment Opportunity
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika

SHULE YA BUPAMWA YAPONGEZWA KWA KUFUTA ZIRO

Posted on: September 7th, 2024


Mkurugenzi wa mipango na sera kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI Ndugu John Mihayo Cheyo ameipongeza shule ya Sekondari Bupamwa kwa kuongeza hali ya ufaulu wa kidato cha nne na kufuta ziro.


Ameyasema hayo kwenye mahafari ya 15 ya Kidato cha nne iliyofanyika tarehe 7,Septemba  2024 Shuleni hapo


" niwapongeze walimu,wanafunzi na viongozi wote mlosimamia uboreshaji wa elimu hadi kufikia kufuta ziro kwa matokeo ya kidato cha nne sasa ongezeni juhudi muondoe daraja la nne" alisema Cheyo


Akiwasilisha taarifa ya shule hiyo Mkuu wa Shule Mwalimu Herman Shingisha alisema Pamoja na mafanikio makubwa ya kupandisha ufaulu shule hiyo bado inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo upungufu wa matenki ya kutunzia maji, bwalo,jengo la utawala,jengo la TEHAMA  na mahitaji mengine.


Ndugu Cheyo ambaye alikuwa mgeni rasmi katika Mahafali hiyo alitatua baadhi ya changamoto za Shule hiyo kama matenki ya maji na sufuria za kupikia chakula cha wanafunzi.


Jumla ya wanafunzi 92 wanatarajiwa kufanya mtihani wa kidato cha nne kati ya wanafunzi 202 walioanza kidato cha kwanza mwaka 2021, ambapo changamoto kubwa katika shule hiyo ni wanafunzi kuacha shule, utoro wa rejareja na wengine kuhama


" tatizo kubwa lililokuwa linasababisha wanafunzi wetu kuacha shule ni umbali maana wapo wanafunzi wanaotembea zaidi ya kilomita 40 kuja na kurudi nyumbani, lakini tatizo limetatuliwa maana shule imeshajengwa huko Kiliwi ambayo inachukua wanafunzi wanaotoka kijiji cha kiliwi, Itegamatu na kijiji cha Dodoma" alisema Mkuu wa Shule Shingisha


Nao wanafunzi wanaotokea vijiji hivyo walieleza jinsi walivyopambana na changamoto hasa kipindi cha masika ambapo mito ikijaa maji walishindwa kufika shuleni " tumepitia wakati mgumu sana maana kutoka nyumbani hadi hapa shule ni mbali sana na kipindi cha mvua kuna mto ambao ukijaa haiwezekani kupita  kuja shuleni  lakini nimepambana, wazazi walinipa baskeli ambayo ilinisaidia"  alisema Justina  Kasangu

Matangazo

  • TANGAZO LA MNADA April 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WANAWAKE,VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 07, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA MAGARI NA PIKIPIKI February 20, 2025
  • TAHADHARI YA KIPINDUPINDU September 12, 2024
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • WANAFUNZI WAHIMIZWA KUSOMA KWA BIDII

    March 21, 2025
  • MKUU WA WILAYA AHIMIZA USAWA WA KIJINSIA NA UWAJIBIKAJI

    March 06, 2025
  • WATENDAJI WATAKIWA KUONGEZA JUHUDI ZA UKUSANYAJI MAPATO

    February 27, 2025
  • KWIMBA YATOA MILIONI 607 KWA VIKUNDI 37 VYA VIJANA,WANAWAKE NA WALEMAVU

    February 21, 2025
  • Onyesha zote

Video

ZIARA YA MHESHIMIWA DC TARAFA YA MWAMASHIMBA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2016
  • Orodha ya watumishi wenye vyeti vya kugushi
  • Orodha ya Madaktari waliojariwa April 2017
  • Ajira mpya za walimu wa Hisabati na Sayansi 2016/2017
  • Matokeo ya Kumaliza Kidato cha Sita na Ualimu 2017

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tovuti ya ofisi ya Rais utumishi wa umma
  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza
  • Tovuti ya ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Tume ya Maadili

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Mawasiliano

    Ngudu-Kwimba

    Sanduku la Posta: P.O.BOX 88

    Namba ya Simu: 0732 980528

    Simu ya Kiganjani: 0732980528

    Barua Pepe: ded@kwimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma zetu

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.