• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kwimba District Council
Kwimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Orodha ya viongozi
      • Orodha ya wenyeviti wa Halmashauri
      • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Orodha ya wakurugenzi
    • Muundo wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na Usafi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Taka na Usafi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Utamaduni, Michezo na Sanaa
      • Kitengo cha Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • TEHAMA
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
      • Elimu
    • Elimu
    • Mkataba wa Hduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari
  • Machapisho
    • Fomu
  • Investment Opportunity
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika

WAKIMBIZA MWENGE WAIPONGEZA KWIMBA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI

Posted on: July 12th, 2022


Mkimbiza Mwenge Kitaifa Ndugu Sahili Nyanzabara Geraruma awapongeza viongozi wa  Wilaya ya Kwimba kwa kusimamia,na kutekeleza miradi ya maendeleo kwa ufanisi na ufasaha.Ndugu Geraruma ameyasema hayo wakati akikagua miradi tisa,ambapo miradi  mitatu imekaguliwa,miradi mitatu imewekewa mawe ya msingi na miradi mitatu imezinduliwa.

Mwenge wa Uhuru umepokelewa  leo tarehe 12,Julai 2022 katika Kijiji cha Mwamhembo kata ya Malya umekimbizwa kilomita 124.8 na umekagua miradi hiyo yenye jumla ya bilioni 3.82. Katika mbio hizo mwenge  ulianza kwa kukagua mradi wa  programu maalumu ya mafunzo kwa wanafunzi wakike waliokatisha masomo baada ya kupata ujauzito katika Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Malya. Katika Chuo hicho wakimbiza mwenge wamewapongeza wanafunzi wote wanaosoma katika chuo hicho na wameshauri kusoma kwa bidii ili wafikie malengo yao.

Aidha mwenge huo umekagua mradi wa anwani za makazi katika kijiji cha Malya ambapo jiwe la msingi limewekwa katika mradi huo, Kisha Mwenge umekagua na kuweka jiwe la msingi katika  mradi wa ujenzi wa tangi la  maji lenye ujazo wa  lita 135,000  katika kijiji cha Ibindo.Mwenge huo haukuishia hapo  umeweka jiwe la Msingi katika  mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya katika kijiji cha Isunga.

Mwenge wa Uhuru umezindua madarasa matano katika Shule ya Sekondari Walla,umezindua daraja la Walla na umezindua madarasa sita katika Shule ya Msingi Kabale ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba kupitia mapato ya ndani imeweza kujenga madarasa ya kisasa sita baada ya madarsa yaliyokuwepo katika Shule hiyo kuchakaa na kutofaa kwa matumizi. Katika miradi hiyo wakimbiza mwenge wamepongeza jitihada zilizofanya na Halmashauri ili kufanikisha ujenzi hio katika Shule ya Msingi Kabale.

Katika mbio hizo wakimbiza Mwenge wa Uhuru wamesisitiza kauli mbiu ya Mwenge wa Uhuru 2022 inayosema”Sensa ni msingi wa mipango ya maendeleo,shiriki kuhesabiwa tuyafikie maendeleo ya Taifa” aidha wakimbiza Mwenge hao wametoa elimu kwa Wananchi juu ya umuhimu wa Sensa ya watu na makazi,wamesisitiza lishe kamili kwa watu wote ili kuepukana na udumavu na utapiamlo.

Matangazo

  • TANGAZO LA MNADA April 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WANAWAKE,VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 07, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA MAGARI NA PIKIPIKI February 20, 2025
  • TAHADHARI YA KIPINDUPINDU September 12, 2024
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • WANAFUNZI WAHIMIZWA KUSOMA KWA BIDII

    March 21, 2025
  • MKUU WA WILAYA AHIMIZA USAWA WA KIJINSIA NA UWAJIBIKAJI

    March 06, 2025
  • WATENDAJI WATAKIWA KUONGEZA JUHUDI ZA UKUSANYAJI MAPATO

    February 27, 2025
  • KWIMBA YATOA MILIONI 607 KWA VIKUNDI 37 VYA VIJANA,WANAWAKE NA WALEMAVU

    February 21, 2025
  • Onyesha zote

Video

ZIARA YA MHESHIMIWA DC TARAFA YA MWAMASHIMBA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2016
  • Orodha ya watumishi wenye vyeti vya kugushi
  • Orodha ya Madaktari waliojariwa April 2017
  • Ajira mpya za walimu wa Hisabati na Sayansi 2016/2017
  • Matokeo ya Kumaliza Kidato cha Sita na Ualimu 2017

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tovuti ya ofisi ya Rais utumishi wa umma
  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza
  • Tovuti ya ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Tume ya Maadili

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Mawasiliano

    Ngudu-Kwimba

    Sanduku la Posta: P.O.BOX 88

    Namba ya Simu: 0732 980528

    Simu ya Kiganjani: 0732980528

    Barua Pepe: ded@kwimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma zetu

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.