• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kwimba District Council
Kwimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Orodha ya viongozi
      • Orodha ya wenyeviti wa Halmashauri
      • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Orodha ya wakurugenzi
    • Muundo wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na Usafi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Taka na Usafi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Utamaduni, Michezo na Sanaa
      • Kitengo cha Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • TEHAMA
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
      • Elimu
    • Elimu
    • Mkataba wa Hduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari
  • Machapisho
    • Fomu
  • Investment Opportunity
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika

WAKIMBIZA MWENGE WAIPONGEZA KWIMBA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI

Posted on: July 19th, 2023



Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2023 Ndugu Abdalla Shaibu Kaim ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa utekelezaji wa Miradi, Uongozi wa Kwimba na Wananchi kwa utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Afya uliozingatia Ubora na Viwango kwenye kijiji cha Budushi.


Ametoa pongezi hizo mapema leo Julai 19, 2023 kwenye Uwekaji wa Jiwe la Msingi la kituo hicho ambacho kinatekelezwa kwa zaidi ya Milioni 315, zikiwemo Milioni 300 kutoka Mapato ya ndani ya Halmashauri ambacho ujenzi wake umeanzishwa na wananchi wa Kijiji cha Budushi kwa kununua Eneo la Ekari Saba pamoja na kuchimba na kujenga Msingi kwa gharama ya Zaidi ya Milioni 15.


"Ukitaka kujua kwamba Mhe. Rais Samia anafanya kazi kubwa kwenye Sekta ya Afya basi njoo ujionee Sumve, ukienda katika vijiji cha Bumengeja, Nyamikoma, Mwashilalage kote kazi za heshima sana zinaendelea na hapo awali wananchi hawakuwahi kupata huduma hizi karibu na makazi yao." Amesema Mhe. Kasalali Mageni, Mbunge wa Sumve (CCM).


Akitoa taarifa ya Ujenzi wa Mradi huo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji, Ndugu Emanuel Lameck ambaye ni Mtendaji wa Kata ya Sumve amefafanua kuwa asili ya Kuanzishwa kwa Ujenzi wa Kituo hicho ni kutokana na wananchi kuchoshwa na Adha ya Msongamano wa Wagonjwa kwenye Hospitali inayomilikiwa na Kanisa Katoriki Sumve.


Ndugu Lameck amefafanua kuwa Ujenzi wa kituo hicho unatekelezwa kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza yanajengwa Majengo ya Wagonjwa Nje (OPD) pamoja na Choo cha nje chenye Matundu Manne ambavyo kwa pamoja Ujenzi wake umefikia 90% na kwamba kwenye awamu ya pili wanatarajia kujenga Wodi za wanawake na wanaume na Kichomea taka.


"Mradi huu unatakiwa kukamilika Julai 30, 2023 na kuanza kutoa huduma za afya kwa wananchi wapatao 72,138 ambapo kata ya Sumve ni wananchi 19,195, Mantare 13,153, Ngulla 13,673, Walla 19,763 pamoja na Mwabomba wananchi 3,192." Amefafanua Mtendaji Kata.


Katika wakati mwingine Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru ameipongeza Kwimba kwa kuanzisha Shamba darasa la Malisho ya Mifugo ambapo wafugaji watapata Ujuzi wa kupanda, kutunza na kuinua uchumi.

Matangazo

  • TANGAZO LA MNADA April 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WANAWAKE,VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 07, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA MAGARI NA PIKIPIKI February 20, 2025
  • TAHADHARI YA KIPINDUPINDU September 12, 2024
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • WANAFUNZI WAHIMIZWA KUSOMA KWA BIDII

    March 21, 2025
  • MKUU WA WILAYA AHIMIZA USAWA WA KIJINSIA NA UWAJIBIKAJI

    March 06, 2025
  • WATENDAJI WATAKIWA KUONGEZA JUHUDI ZA UKUSANYAJI MAPATO

    February 27, 2025
  • KWIMBA YATOA MILIONI 607 KWA VIKUNDI 37 VYA VIJANA,WANAWAKE NA WALEMAVU

    February 21, 2025
  • Onyesha zote

Video

ZIARA YA MHESHIMIWA DC TARAFA YA MWAMASHIMBA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2016
  • Orodha ya watumishi wenye vyeti vya kugushi
  • Orodha ya Madaktari waliojariwa April 2017
  • Ajira mpya za walimu wa Hisabati na Sayansi 2016/2017
  • Matokeo ya Kumaliza Kidato cha Sita na Ualimu 2017

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tovuti ya ofisi ya Rais utumishi wa umma
  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza
  • Tovuti ya ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Tume ya Maadili

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Mawasiliano

    Ngudu-Kwimba

    Sanduku la Posta: P.O.BOX 88

    Namba ya Simu: 0732 980528

    Simu ya Kiganjani: 0732980528

    Barua Pepe: ded@kwimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma zetu

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.