Wananchi wameaswa kuendeleza ushirikiano na umoja ulioanzishwa na viongozi waasisi wa Taifa hili, haya yamesemwa na Ndugu. John Mihayo Cheyo Mkurugenzi kutoka TAMISEMI ambaye alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa Albamu ya Kwaya ya AIC Ngudu
"kama huwezi kuhubiri au kuimba basi changia fedha ili kupitia uimbaji wao watu wamjue Mungu na Taifa liendelee kuishi kwa amani, niwasihi wote mliofika hapa tujitoe kushiriki kuiinua kwaya hii ili ienndelee kuhubiri kupitia nyimbo" amesema Cheyo
Katika uzinduzi huo wameshiriki viongozi mbalimbali akiwemo Katibu Tawala Wilaya ya Kwimba Ndugu Mohamed Ngasinda ambaye amewataka wananchi kuendelea kuuenzi Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
" niwapongeze wanakwaya wote mmeimba vizuri, lakini nitumia nafasi hii kuwakumbusha wananchi wote kuwa jana ilikuwa siku ya kumbukizi ya Muungano kwahiyo tuendelee kulinda umoja wetu, tusiruhusu watu wavunje amani yetu, wanakwimba ni wamoja tuendeleze umoja huu" pia amewaasa wanakwaya hao kuendelea kusimamia mipango yao kwa uadilifu na uaminifu.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba Dkt Amon Mkoga amewapongeza wanakwaya hao kwa hatua hiyo ya kuzindua albamu ya nyimbo za injili na amewaahidi ushirikiano pindi watakapohitaji kufanya jambo linalohitaji usaidizi wake " nimefurahi sana kushirikiriki uzinduzi huu na niwapongeze kwa hatua hii, pia nimeskia kwenye risala yenu mnataka kuanzisha shule ya awali niwakaribishe ofisini kwangu kwaajili ya ushauri" Mkoga
Awali Mchungaji wa kanisa hilo Mchungaji Mathias Mleka amewataka waumini na wanakwaya walioshiriki uzinduzi huo kuzingatia mambo makuu matano " kama mnataka kazi zenu kufanikiwa zingatieni haya umoja,uwazi,uwajibikaji,uadilifu na uaminifu mkiyazingatia haya mtafikisha injili kwa watu wote" amesema Mchungaji huyo
Ngudu-Kwimba
Sanduku la Posta: P.O.BOX 88
Namba ya Simu: 0732 980528
Simu ya Kiganjani: 0732980528
Barua Pepe: ded@kwimbadc.go.tz
Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.