• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kwimba District Council
Kwimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Orodha ya viongozi
      • Orodha ya wenyeviti wa Halmashauri
      • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Orodha ya wakurugenzi
    • Muundo wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na Usafi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Taka na Usafi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Utamaduni, Michezo na Sanaa
      • Kitengo cha Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • TEHAMA
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
      • Elimu
    • Elimu
    • Mkataba wa Hduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari
  • Machapisho
    • Fomu
  • Investment Opportunity
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika

WANANCHI WATAKIWA KUIMARISHA NYUMBA ZAO ILI KUJIKINGA NA MAJANGA

Posted on: October 9th, 2023



Umekuwa utaratibu wa baadhi ya watu wanaoishi maeneo ya vijijini kujenga nyumba na kuzipaua kwa bati bila kupigilia misumari ili kushikiza bati na mbao badara yake mawe ndio yanawekwa juu ya bati, jambo hili limeonekana kuwa ni hatari hasa pindi mvua za upepo zitakaponyesha mawe hayo yanaweza kusababisha majanga.


Kutokana na hali hiyo Mkuu wa Wilaya ya Kwimba Mheshimiwa Ng'wilabuzu Ludigija amewataka Wananchi ambao wamejenga nyumba na kuziwekea mawe juu ya bati, kuondoa mawe hayo na mabati yapigiliwe misumari Ili kujiepusha na majanga yanayoweza kuzuirika


" niwaombe Wananchi wenye nyumba za (slop) imarisheni nyumba zenu, tumieni misumari badara ya mawe maana tumeshaambiwa mvua za mwaka huu zitakuwa kubwa huenda zikawa na upepo unaoweza kusababisha hayo mawe yakawaangukia waliolala ndani" amesema Ludigija


Mkuu wa Wilaya ameyasema hayo leo Oktoba 9,2023 wakati akisikiliza na kutatua kero za wananchi wa Kata ya Bugando na Iseni.


Aidha Mheshimiwa Ludigija amewasisitiza wananchi wa Kata ya Bugando kuhamasisha watoto wao kupenda Shule kwani Kata hiyo imeonekana kuwa na changamoto ya utoro hasa kwa wanafunzi wa Sekondari


"wazazi wahamasisheni watoto kwenda Shule waache utoro, tambueni kuwa Elimu ndiyo urithi pekee utakaomsaidia mtoto wako siyo mashamba ambayo yanasababisha migogoro ya ardhi kila siku" Ludigija


Katika ziara hiyo Mkuu wa Wilaya ametatua changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa maji,umeme, migogoro ya Ardhi pia amewahamasisha wazazi kuchangia vyakula ili wanafunzi wapate chakula shuleni.


Naye Diwani wa Kata ya Bugando Mheshimiwa Chenyenge ameitumia nafasi hiyo kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuleta fedha nyingi za kutekeleza miradi ya Elimu, maji na Barabara.

Matangazo

  • TANGAZO LA MNADA April 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WANAWAKE,VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 07, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA MAGARI NA PIKIPIKI February 20, 2025
  • TAHADHARI YA KIPINDUPINDU September 12, 2024
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • WANAFUNZI WAHIMIZWA KUSOMA KWA BIDII

    March 21, 2025
  • MKUU WA WILAYA AHIMIZA USAWA WA KIJINSIA NA UWAJIBIKAJI

    March 06, 2025
  • WATENDAJI WATAKIWA KUONGEZA JUHUDI ZA UKUSANYAJI MAPATO

    February 27, 2025
  • KWIMBA YATOA MILIONI 607 KWA VIKUNDI 37 VYA VIJANA,WANAWAKE NA WALEMAVU

    February 21, 2025
  • Onyesha zote

Video

ZIARA YA MHESHIMIWA DC TARAFA YA MWAMASHIMBA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2016
  • Orodha ya watumishi wenye vyeti vya kugushi
  • Orodha ya Madaktari waliojariwa April 2017
  • Ajira mpya za walimu wa Hisabati na Sayansi 2016/2017
  • Matokeo ya Kumaliza Kidato cha Sita na Ualimu 2017

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tovuti ya ofisi ya Rais utumishi wa umma
  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza
  • Tovuti ya ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Tume ya Maadili

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Mawasiliano

    Ngudu-Kwimba

    Sanduku la Posta: P.O.BOX 88

    Namba ya Simu: 0732 980528

    Simu ya Kiganjani: 0732980528

    Barua Pepe: ded@kwimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma zetu

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.