• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kwimba District Council
Kwimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Orodha ya viongozi
      • Orodha ya wenyeviti wa Halmashauri
      • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Orodha ya wakurugenzi
    • Muundo wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na Usafi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Taka na Usafi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Utamaduni, Michezo na Sanaa
      • Kitengo cha Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • TEHAMA
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
      • Elimu
    • Elimu
    • Mkataba wa Hduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari
  • Machapisho
    • Fomu
  • Investment Opportunity
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika

WANANCHI WATAKIWA KUTUMIA KAMATI YA USHAURI WA KISHERIA ILI KUONDOA MALALAMIKO

Posted on: April 22nd, 2025


Mkuu wa Wilaya ya Kwimba Mhe. Ng'wilabuzu Ludigija amewataka Wananchi kutumia kamati ya ushauri wa kisheria katika kutatua kero na malalamiko dhidi ya Serikali na malalamiko kati ya mtu na mtu.


Mkuu wa Wilaya ameyasema hayo leo April  22,2025 kwenye uzinduzi wa kamati ya ushauri wa kisheria ambayo ameizindua rasmi huku akisisitiza kamati hiyo kwenda kutatua Malalamiko ya Wananchi ili kupunguza mlundikano wa kesi mahakamani na kuondoa malalmiko ya wananchi dhidi ya Serikali 


" Lengo kuu la Serikali kuanzisha Kamati hii ni kuwapunguzia kero na malalamiko hasa yanayolenga Serikali lakini na yanayowalenga wananchi wenyewe, kwahiyo niwaombe wote mlioshiriki hapa mkawe mabalozi kuwahamasisha wananchi  kutumia kamati hii kutatua changamoto zao"


Aidha ametumia wasaa huo kuilitambulisha dawati la msaada wa kisheria ambalo linafanya kazi chini ya kampeni ya msaada wa kisheria wa  Mama Samia " pia hapa tuna watu wanaofanya kazi kwenye dawati la msaada wa kisheria watumieni" Ludigija 


Akiwasilisha taarifa fupi ya kazi  Mwenyekiti wa Kamati hiyo Bi. Helen Chuma Wakili wa Serikali amesema kamati hiyo itakuwa na majuku mbalimbali ikiwa ni pamoja na kupunguza au kuondoa malalamiko kwa wananchi dhidi ya Serikali, kutoa elimu na kuhamasisha swala la haki na wajibu


" kamati itapokea malalamiko yenye uhalisia wa kile kinacholalamikiwa" amesema Helen


Wajumbe walioshiriki uzinduzi huo wameipongeza Serikali kwa kuanzisha kamati hiyo na wameshauri kamati ifanye kazi kwa kuanza na changamoto za wazi hasa kero ya ajari zinazosababishwa na waendesha pikipiki wasiozingatia sheria za usalama barabarani


" Mkuu wa polisi (W) Kwimba tunaomba aongeze jitihada za usalama barabarani ili hawa waendesha pikipiki wasimamiwe ajari zinaongezeka tunazika watu kwaajili ya ajari za pikipiki hili limetuchosha" amesema Julias Nyerere Mwenyekiti wa Chama cha walemavu


Serikali ya awamu ya sita inaendelea kutatua kero na changamoto za wananchi kwa kuanzisha dawati la msaada wa kisheria na kamati ya msaada wa kisheria ambapo wote wanalenga kumsaidia mwananchi kupata haki na kutatua changamoto bila kutumia gharama kubwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA MNADA April 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WANAWAKE,VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 07, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA MAGARI NA PIKIPIKI February 20, 2025
  • TAHADHARI YA KIPINDUPINDU September 12, 2024
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • WAZIRI MKUU AWEKA JIWE LA MSINGI JENGO LA UTAWALA LA HALMASHAURI

    May 18, 2025
  • WAUGUZI WATAKIWA KUENDELEA KUTOA HUDUMA BORA

    May 12, 2025
  • MAADHIMISHO YA MEIMOSI YAHAMASISHA WANANCHI KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU

    May 01, 2025
  • MKURUGENZI AWATAKA WATUMISHI WOTE KUFANYA KAZI KWA UPENDO NA UADILIFU

    April 28, 2025
  • Onyesha zote

Video

ZIARA YA MHESHIMIWA DC TARAFA YA MWAMASHIMBA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2016
  • Orodha ya watumishi wenye vyeti vya kugushi
  • Orodha ya Madaktari waliojariwa April 2017
  • Ajira mpya za walimu wa Hisabati na Sayansi 2016/2017
  • Matokeo ya Kumaliza Kidato cha Sita na Ualimu 2017

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tovuti ya ofisi ya Rais utumishi wa umma
  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza
  • Tovuti ya ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Tume ya Maadili

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Mawasiliano

    Ngudu-Kwimba

    Sanduku la Posta: P.O.BOX 88

    Namba ya Simu: 0732 980528

    Simu ya Kiganjani: 0732980528

    Barua Pepe: ded@kwimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma zetu

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.