• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kwimba District Council
Kwimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Orodha ya viongozi
      • Orodha ya wenyeviti wa Halmashauri
      • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Orodha ya wakurugenzi
    • Muundo wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na Usafi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Taka na Usafi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Utamaduni, Michezo na Sanaa
      • Kitengo cha Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • TEHAMA
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
      • Elimu
    • Elimu
    • Mkataba wa Hduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari
  • Machapisho
    • Fomu
  • Investment Opportunity
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika

Kilimo cha Pamba, Mpunga, Dengu na Choroko


                                                               Kilimo cha Pamba Kinavyotekelezwa Wilayani Kwimba

1.0: HISTORIA YA KILIMO CHA ZAO LA PAMBA WILAYANI KWIMBA

Pamba ni zao kuu la biashara katika wilaya ya Kwimba zaidi ya asilimia 70 ya wakulima walikuwa wanajishughulisha na kilimo cha pamba.  Kwa kipindi cha miaka mitatu zao la pamba limekuwa likishuka uzalishaji kama ifuatavyo; mwaka 2014/2015 uzalishaji ulikuwa kilo 7,596,916, 2015/2016, kilo 4,512,420 na 2016/2017 kilo 2,051,122.

Katika vipindi vyote hivi vitatu kulikuwepo na mafanikio na changamoto mbalimbali zilizojitokeza. Mafanikio machache yaliyopatika kupitia kilimo cha pamba kwa mkataba ni upatikanaji wa pembejeo kwa mkopo, uwezeshwaji wa huduma za ugani kutoka kwa makampuni na  uundaji wa Vikundi vya wakulima (FBGs). Mbali na mafanikio machache kulikuwa na changamoto zilizokwamisha kilimo cha mkataba zikiwemo; ukopeshwaji usio fuata taratibu, urejeshwaji mdogo wa madeni, pembejeo zisizo na ubora, makampuni kushindwa kutimiza masharti ya mkataba, bei ya dogo ukilinganisha na gharama za uzalishaji na mvua zenye mtawanyiko usioridhisha.

2.0: UTEKELEZAJI WA KILIMO CHA PAMBA KWA MKATABA MSIMU      2016/17

Katika msimu wa kilimo cha pamba 2016/17, Wilaya ya Kwimba imeitikia wito wa Mhe.Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufufua zao la pamba ambalo kwa takribani miaka mitano uzalishaji wake umeshuka. Lengo ni kuwezesha uzalishaji mkubwa wa pamba kama malighafi wenye tija ili kuwezesha uendeshaji wa viwanda.Kwa kutambua kuwa zao hili lina mnyororo mrefu wa thamani.

Katika kutekeleza agizo la Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John .V.K.Mongella, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza aliagiza Wakuu wa Wilaya kuhakikisha zao la pamba linafufuliwa kwa kuongeza tija na uzalishaji. Wilaya ya Kwimba iliandaa andiko lenye vigezo na masharti ya kuwekeza katika kilimo cha pamba na kulituma kwa Makampuni 13 ambayo ni  Afrisian Ginning, SM Holdings, ICK Cotton, Kahama  Oil Mills, Kahama Cotton Company, Alliance Ginneries, Birchad Oil Mills, Olam (T), Aham Investment Co. Ltd, Fresho Investment, Gaki Investment Co. Ltd na Nida Textile Mill. Makampuni hayo yalitumiwa mwaliko wa kuomba kuwekeza katika kilimo cha pamba kwa mkataba kuanzia msimu 2016/2017. Kati ya makampuni 13 ni makampuni matatu (3) ambayo ni SM Holdings, Afrisian Ginning na ICK Cotton ziliomba  kuwekeza na baadaye Halmashauri ilifunga mkataba na kampuni hizo kwa kipindi cha miaka mitatu.

 

 3.0: MIKAKATI ILIYOTUMIKA KUFANIKISHA KILIMO CHA MKATABA

Timu za uhamasishaji wa ngazi ya Wilaya kupita kila kijiji kuelemisha na kuamsha ari ya kufufua kilimo cha pamba walau kila kaya kulima ekari moja.

Ushirikishwaji wa wadau mbalimbali katika shughuli za kilimo cha pamba hususan Bodi ya Pamba, TGT na wataalam kutoka kampuni Quton.

Kugawa maeneo ya uwekezaji kwa kuzingatia mahitaji ya Kampuni; SM Holdings tarafa ya Ibindo, Afrisian Ginning tarafa ya Mwamashimba na ICK Cotton tarafa ya Nyamilama, Ngudu na Ngulla. Lengo la Wilaya kugawa uwekezaji kwa maeneo ni kuondoa muingiliano na utegeaji katika uwekezaji.

Uundwaji wa Vikosi Kazi ngazi ya Wilaya na Vijiji kwa lengo la kusimamia utekelezaji wa kilimo cha pamba.

Kuboresha huduma za ugani kwa kuwapa maafisa ugani pikipiki, mafuta na posho kwa ajili ya kusimamia majukumu yao.

Kuanzisha shamba darasa la viongozi wa kamati ya Ulinzi na Usalama na Wakuu wa Idara wa Halmashauri ili kuhamasisha jamii kutekeleza kilimo cha Pamba.

Kuanzisha mashamba darasa katika shule za msingi na  Sekondari ili kufufua elimu ya kujitegemea shuleni na kuandaa wakulima wa baadaye.

Usimamizi thabiti wa utekelezaji wa majukumu yaliyoanishwa kwenye mkataba.

 

4.0: HALI YA USAMBAZAJI PEMBEJEO

Kwa msimu 2016/17, Wilaya ilipata mgawo wa mbegu tani 500 UK 91(manyoya) kutoka Bodi ya pamba. Kutokana na mahitaji kuongezeka hadi kumalizika kwa msimu wa kupanda jumla ya tani 518 za UK 91 na tani 80 za UKM08 (kipara) zilisambazwa vijijini. Kati ya mbegu hizo jumla ya tani 488 za UK 91 na tani 78 za UKM08 zilichukuliwa na wakulima. Makisio ya ekari zilizotarajiwa kulimwa zilikuwa ni ekari 61,873.

 Kutokana na changamoto ya hali ya hewa ilisababisha wakulima kulazimika kupanda zaidi ya mara moja na wengine kushindwa kabisa kupanda. Makisio  yalishuka hadi kufikia ekari 46,000. Hata hivyo katika zoezi la uhakiki wa mashamba ambalo limekamilika mwezi Machi, jumla ya ekari 24,025 zimebainishwa kupandwa na kuota vizuri.

 Kulingana na makisio ya ekari 61,873 ambazo zilitokana na usambazaji wa mbegu, mahitaji ya viuadudu yalikuwa chupa 165,000. Hadi kufikia sasa ni chupa 59,040 ambazo zimesambazwa vijijini, kati ya viuadudu hivyo chupa 46,840 zimetolewa na makampuni, chupa 11,500 zimetolewa na CDTF na chupa 700 zimetolewa na Bodi ya Pamba. Kwa upande wa vinyunyizi jumla ya vinyunyizi 189 vimesambazwa na vinyunyizi 148 vimechukuliwa na wakulima.

4.1:  Ukopeshwaji wa pembejeo kwa kila kampuni

KAMPUNI
MBEGU
DENI  LA MBEGU (TShs)
VIUADUDU (CHUPA)
DENI LA VIUADUDU
WAKULIMA WALIOKOPA MBEGU (Idadi)
UK 91
UK M08
SM HOLDINGS
91,387
47,856
173,760,500/=
14,068
28,136,000/=
5,472
I.C.K COTTON
227,237
0
167,070,128/=
22,803
45,606,000/=
5,493
AFRISIAN GINNING
123,650
30,178
104,415,500/=
10,034
20,068,000/=
3,193
JUMLA
442,276
77,396
444,618,128/=
46,905
93,810,000/=
14,158

Jumla ya Tsh 538,428,128.00 zimewekezwa na makampuni matatu zikiwa ni gharama ya mbegu na viuadudu.

5.0: UWEZESHWAJI WA SHUGHULI ZA KILIMO CHA PAMBA KWA MKATABA.

Katika kuendesha shughuli za kilimo cha pamba kwa mkataba, Halmashauri imechangia shilingi milioni 7.3 ambazo zilitumika katika zoezi la uhamasishaji wa  kilimo cha pamba kwa kununua mafuta ya dizeli na petroli. Wilaya ilipokea pikipiki 10 na shilingi milioni 12 kutoka kwa makampuni, Shirika lisilokuwa la kiserikali la Gatsby Africa liliwezesha shilingi milioni 8. Fedha hizo zimekuwa na mchango mkubwa katika kufanikisha shughuli za kilimo cha pamba hususan katika mambo yafutayo;

  • Posho ya nauli na mafuta kwa maafisa ugani, uendeshaji wa vikao vya kazi vya maafisa ugani ambavyo vimeweza kufanyika mara mbili, hii ni katika kuhakikisha kuwa elimu ya kilimo bora cha pamba inawafikia wakulima kwa wakati
  • Kusimamia zoezi la uhakiki wa mashamba yaliyolimwa na kuota vizuri
  • Mafuta ya dizeli kwa ajili ya maafisa kilimo wilayani na wajumbe wa DTF kufika vijijini kufuatilia taarifa mabalimbali za maendeleo ya kilimo na kufanya mazunguzo na Vikosi kazi vya pamba vya vijiji na wakulima.


6.0: MAFANIKIO KUPITIA KILIMO CHA PAMBA KWA MKATABA.

  • Ushirikiano mzuri baina ya viongozi ngazi zote Wilayani zimeleta matarajio makubwa ya kufufua zao la pamba.
  • Mwitikio mkubwa wa wakulima kulima pamba bila kukata tamaa kwa changamoto ya hali ya hewa.
  • Kumekuwepo na msingi mzuri wa VTF, katika kuunda na VTF kutambua wajibu wao katika kusimamia usambazaji wa pembejeo na kuhakikisha kuwa pembejeo zinafika kwa wakati na zinamfikia mkulima katika eneo lake.
  • Wilaya ilipokea pikipiki 10 kutoka kwa makampuni 3 na kuwagawia maafisa ugani ambao hawakuwa na pikipiki kwa ajili ya kusimamia shughuli za pamba.
  • Wilaya ilipata tani 80 za mbegu ya UKM08 ambayo ni mbegu, mpya na bora kwa kuwa inatoa matunda mengi ambayo yanaongeza tija katika uzalishaji na kuhamasisha wakulima.
  • Kupata pembejeo za kilimo kwa muda muafaka kulingana na mahitaji.
  • Kutatua changamoto za kilimo cha pamba kwa haraka kwa kuwa DTF na kampuni huketi kila wiki, kuangalia mapungufu mbalimbali ambayo yanajitokezea na kuyatolea ufumbuzi wa haraka ili kuepuka athari kubwa kwa mkulima.
  • Kurudisha fikra za wakulima katika kilimo cha pamba kwa kuwa pembejeo zimekuwa zinapatikana kwa wakati na kwa urahisi. Takribani 95% ya wakulima waliolima pamba katika msimu huu wamekopa pembejeo.
  • Maafisa ugani wa kata walijengewa uwezo na kampuni ya uzalisha wa mbegu ya Quton
  • Kuanzisha mashamba darasa katika shule za Msingi na Sekondari
  • Tunarajia kuongeza uzalisha kutoka kilo 2,051,122 hadi kufikia kilo 9,610,00

7.0: CHANGAMOTO

  • Upungufu wa mvua kwa mwezi Desemba na Januari ulisababisha wakulima wengi kushindwa kupanda mbegu ya pamba na wengine ambao walikuwa wameshapanda kurudia tena kutokana na mbegu walizopanda mara ya kwanza kutoota kabisa. Baadhi ya wakulima walitelekeza mashamba yao.
  • Zao la pamba kunyauka na kudondosha majani na vitumba ambavyo havijakomaa kutokana na kushambuliwa na wadudu  aina ya ‘thrips’
  • Upungufu wa maafisa ugani.
  • Kuwa na aina nyingi ya viuadudu katika soko na vingine kutokuwa uwezo wa kuua wadudu kama perfector, Turantura na snowmectic

8.0: MIKAKATI

  • Kikosi Kazi cha Pamba cha Wilaya kulinda kampuni ambazo zimewekeza kwa kusimamia mikataba ya uwekezaji.
  • Kikosi Kazi cha Pamba cha Wilaya, Makampuni na VTF kudhibiti utoroshwaji na ununuzi pamba holela
  • Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya na Halmashauri  kudhibiti utoroshwaji na usafirishaji wa pamba zaidi ya saa 12 jioni.
  • DTF, VTF na Wakulima kusimamia usafi, ubora wa pamba, kudhibiti wizi kupitia mizani, kukusanya takwimu za manunuzi na masafirisho pia kukusanya madeni ya pembejeo zilizokopeshwa vijijini.

Matangazo

  • TANGAZO LA MNADA April 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WANAWAKE,VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 07, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA MAGARI NA PIKIPIKI February 20, 2025
  • TAHADHARI YA KIPINDUPINDU September 12, 2024
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • WANAFUNZI WAHIMIZWA KUSOMA KWA BIDII

    March 21, 2025
  • MKUU WA WILAYA AHIMIZA USAWA WA KIJINSIA NA UWAJIBIKAJI

    March 06, 2025
  • WATENDAJI WATAKIWA KUONGEZA JUHUDI ZA UKUSANYAJI MAPATO

    February 27, 2025
  • KWIMBA YATOA MILIONI 607 KWA VIKUNDI 37 VYA VIJANA,WANAWAKE NA WALEMAVU

    February 21, 2025
  • Onyesha zote

Video

ZIARA YA MHESHIMIWA DC TARAFA YA MWAMASHIMBA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2016
  • Orodha ya watumishi wenye vyeti vya kugushi
  • Orodha ya Madaktari waliojariwa April 2017
  • Ajira mpya za walimu wa Hisabati na Sayansi 2016/2017
  • Matokeo ya Kumaliza Kidato cha Sita na Ualimu 2017

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tovuti ya ofisi ya Rais utumishi wa umma
  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza
  • Tovuti ya ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Tume ya Maadili

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Mawasiliano

    Ngudu-Kwimba

    Sanduku la Posta: P.O.BOX 88

    Namba ya Simu: 0732 980528

    Simu ya Kiganjani: 0732980528

    Barua Pepe: ded@kwimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma zetu

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.