• Mawasiliano |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kwimba District Council
Kwimba District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Orodha ya viongozi
      • Orodha ya wenyeviti wa Halmashauri
      • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Orodha ya wakurugenzi
    • Muundo wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira na Usafi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Taka na Usafi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Utamaduni, Michezo na Sanaa
      • Kitengo cha Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • TEHAMA
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
      • Elimu
    • Elimu
    • Mkataba wa Hduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari
  • Machapisho
    • Fomu
  • Investment Opportunity
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika

MABALOZI WA FISTULA WAASWA KUTOA ELIMU

Posted on: September 15th, 2020

Afisa mradi wa fistula Dkt.Magdalena Dalla kutoka shirika la AMREF akifanya ufuatiliaji wa kazi za uelimishaji kuhusu fistula ya uzazi amewataka mabalozi wa fistula kufanya kazi ya kuwaelimisha watu kuhusu fistula ya uzazi na kuibua wahanga wenye tatizo la fistula ili wapelekwe Hospitali ya Bugando kwa ajili ya kufanyiwa matibabu.Akiongea na mabalozi hao Dkt.Dalla amesema fistula ni tundu lisilo la kawaida linalotokea Kati ya kibofu cha mkojo au njia ya haja kubwa na uke au vyote kwa pamoja na kusababisha kutokwa na mkojo au haja kubwa bila kujitambua.



Dkt.Dalla amesema mabalozi wa fistula wanapaswa kutoa elimu hiyo ili wahanga wasaidiwe matibabu ambapo wafadhili wametoa fedha ili wahanga wa fistula wafanyiwe upasuaji bure katika Hospitali ya Bugando Mwanza au CCBRT Dar es salaam.

Aidha Dkt Dalla amewashauri mabalozi wanapotoa elimu ya fistula wasisitize kuwa fistula siyo ugonjwa wa kulongwa(kishirikina) Kama wananchi wengi wanavouchukulia bali niugonjwa unaosababishwa na uzazi pingamizi.


Katika zoezi hilo la ufuatiliaji wa kazi za mabalozi wa fistula Bi.Nakaniwa Mshana Afisa ufuatiliaji wa mradi wa fistula kutoka shirika la MAPERECE amewashauri mabalozi kujitolea kuwafikisha wahanga katika vituo vya Afya au Zahanati ili wanapofika hapo  wasaidiwe jinsi ya kufika  Hospitali ya Bugando kwaajili ya upasuaji. Nakaniwa ameeleza kuwa wahanga wanapofika Bugando kwaajili ya matibabu ya fistula wanahudumiwa bure na nauli wanazotumia wahanga kufika Bugando wanarudishiwa.Nakaniwa amewataka mabalozi wawashauri wahanga kufika Hospitali kwani fistula inatibika.


Wakielezea taarifa za kazi walizozifanya mabalozi wa fistula, wameeleza jinsi walivyoweza kuibua wahanga 23 wa fistula ambapo wahanga 16 niwapya kwa maana kwamba walikuwa hawajapata matibabu yoyote hivyo utaratibu wa kuwafikisha Bugando kwa matibabu umeshafanyika baadhi yao wanaendelea na matibabu  na wahanga 7 wamekutwa wakiwa walishatibiwa miaka mingi iliyopitana.

Hii ni kanga wanayopewa wahanga wa fistula wanaokwenda Bugando kufanyiwa matibabu.

Wananchi wote wanapaswa kutowaficha,kutowatenga wala kutowanyanyapaa wagonjwa wa fistula kwani hilo ni tatizo linaloweza kumpata mwanamke yeyote anayepata uzazi pingamizi wakati wa kujifungua.Pia wanawake wanashauliwa kujifungulia katika vituo vya Afya au Hospitali ili kuepuka kupata tatizo la fistula.

Matangazo

  • TANGAZO LA MNADA April 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WANAWAKE,VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 07, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA MAGARI NA PIKIPIKI February 20, 2025
  • TAHADHARI YA KIPINDUPINDU September 12, 2024
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • WAZIRI MKUU AWEKA JIWE LA MSINGI JENGO LA UTAWALA LA HALMASHAURI

    May 18, 2025
  • WAUGUZI WATAKIWA KUENDELEA KUTOA HUDUMA BORA

    May 12, 2025
  • MAADHIMISHO YA MEIMOSI YAHAMASISHA WANANCHI KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU

    May 01, 2025
  • MKURUGENZI AWATAKA WATUMISHI WOTE KUFANYA KAZI KWA UPENDO NA UADILIFU

    April 28, 2025
  • Onyesha zote

Video

ZIARA YA MHESHIMIWA DC TARAFA YA MWAMASHIMBA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2016
  • Orodha ya watumishi wenye vyeti vya kugushi
  • Orodha ya Madaktari waliojariwa April 2017
  • Ajira mpya za walimu wa Hisabati na Sayansi 2016/2017
  • Matokeo ya Kumaliza Kidato cha Sita na Ualimu 2017

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tovuti ya ofisi ya Rais utumishi wa umma
  • Tovuti ya ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza
  • Tovuti ya ofisi ya Rais Ikulu
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Tume ya Maadili

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Mawasiliano

    Ngudu-Kwimba

    Sanduku la Posta: P.O.BOX 88

    Namba ya Simu: 0732 980528

    Simu ya Kiganjani: 0732980528

    Barua Pepe: ded@kwimbadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma zetu

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.